Mwambegele

Wednesday, May 16, 2007

Muujiza wa Lincoln na Kennedy




Hivi umewahi kusikia muujiza wa hadithi inayozunguka vifo na maisha ya Abraham Lincoln na John Fitzgerald Kennedy? Hebu soma hapa

Abraham Lincoln alichaguliwa kuingia Bunge la Congress mwaka 1846.
John Fitzgerald Kennedy alichaguliwa kuingia Bunge la Congress mwaka 1946.

Abraham Lincoln alichaguliwa kuwa Rais mwaka 1860.
John Fitzgerald Kennedy alichaguliwa kuwa Rais mwaka 1960.

Wote wawili walijihusisha na haki za raia (civil rights).
Wote wawili walifiwa watoto wakiwa Ikulu.

Wote wawili waliuawa kwa kupigwa risasi siku ya ijumaa.
Wote wawili walipigwa risasi kichwani.

Katibu Muhtasi wa Lincoln aliitwa Kennedy.
Katibu Muhtasi wa Kennedy aliitwa Lincoln (hata hivyo madai haya huwa yanabishaniwa ona kwa mfano hapa http://home.comcast.net/~sharonday7/Presidents/AP070102.htm)

Wote waliuawa na watu kutoka kusini ya Marekani.
Baada ya vifo vyao, Wote walifuatiwa na Marais kutoka kusini ya Marekani kwa jina la Johnson.

Andrew Johnson, aliyechukuwa nafasi ya Lincoln baada ya kifo chake, alizaliwa mwaka 1808.
Lyndon Johnson, aliyekuwa Rais baada ya kifo cha Kennedy, alizaliwa mwaka1908.

John Wilkes Booth, aliyemuua Lincoln, alizaliwa mwaka 1839.
Lee Harvey Oswald, muuaji wa Kennedy, alizaliwa mwaka 1939.

Wauaji wao walijulikana kwa majina matatu.
majina ya wauaji wote wawili yana herufi kumi na tano.

Lincoln aliuawa kwenye ukumbi ulioitwa 'Ford.'
Kennedy aliuawa ndani ya gari iliyoitwa ' Lincoln', gari hili lilitengenezwa na 'Ford.'

Lincoln alipigwa risasi ndani ya ukumbi na muuaji wake akakimbilia kujificha kwenye ghala
Kennedy alipigwa risasi kutoka kwenye ghala na baada ya kumuua akakimbilia kujificha ukumbini

Booth na Oswald waliuawa kabla ya kushtakiwa

na kifuatacho labda ni exaggeration ya wasomaji:

wiki moja kabla ya kupigwa risasi, Lincoln alikuwa mji ulioitwa Monroe, Maryland
Wiki moja kabla ya kupigwa risasi Kennedy alikuwa na Marilyn Monroe.

chanzo: mtandao

0 Comments:

Post a Comment

<< Home